About

Friday, March 2, 2012

BIBI MWANAFUNZI MWENYE WA MIAKA 90 !



Akiwa nyumbani kwake na Mwalimu ambae ni sawa na mjukuu wake 
Nyumba anayoishi.
Mwanafunzi mwenye umri mkubwa ambae kuna uwezekano akaingia kwenye kitabu cha kumbukumbu Duniani kutokana na umri wake lakini yuko shuleni, bibi Priscillah Sitienei maarufu kama Gogoo mwenye umri wa miaka 90, ameamplfy kwamba anaenjoy kuanza shule na tayari ameanza kuona mafanikio makubwa na yenye tofauti  kuhusu skonga.
Akiwa darasani na wanafunzi wenzake.
Toka ameanza kusoma mwaka jana huko Kenya, mpaka sasa bibi huyo amethibitisha kwamba kuna mwanga wa mafanikio ameuona, sasa hivi anajua kusoma na kuandika, tofauti na mwaka jana. 
Akiwa darasani na wanafunzi wenzake.
  
Mafanikio ya mwanga aliouona hayajatajwa na yeye peke yake, hata walimu wake wamethibitisha mabadiliko kwake wakisema mwanzoni alikua nashikiwa kalamu lakini sasa anashika mwenyewe.

Yani mpaka sasa bibi priscila anauwezo wa kuongoza darasa ambalo wanafunzi wengine waliobaki ni kama vitukuu vyake, tayari anaweza kusoma baadhi ya maneno ya kiingereza kama Apple, Lion, Mango n.k

NTV KENYA wamesema Bibi huyu mwenye umri wa miaka 90, anasema ni ukweli kwamba ana enjoy kuwepo darasani kila wakati manake hata hao wanafunzi wenzake ambao ni sawa na vitukuu vyake wanampenda na wanampa ushirikiano, wanamuazima vitu kama vile kalamu na anapokosa kwenda shule huwa watoto wanakosa furaha.

Priscillah amesema hajui ataishia wapi kwenye swala la kusoma ila anachomuomba Mungu ni kulinda macho yake ili asishindwe kusoma vitabu.
Msikilize Bibi mwenyewe akiongea hapo chini…..

Facebook comments brought to you by bongo6